Jumapili: Kuwaagiza wale 70 — Luka 10:1-16
Yesu alikuwa akijiandaa kuacha huduma yake duniani, na alikuwa akiwaandaa wanafunzi wake kuendelea na kazi baada ya kuondoka kwake. Alipowaagiza wale 70, alikuwa akiweka mfumo na miongozo ya kushuhudia. Wanafunzi waliagizwa kutoka wawili wawili, hivyo kuunda msingi wa maombi, mafundisho, na uwajibikaji. Waliambiwa waweke tegemeo lao kamili la riziki na makazi mikononi mwa Mungu. Yesu aliwaelezea jinsi ya kushughulikia hali ambapo walikaribishwa kwa uchangamfu nyumbani na jinsi ya kushughulikia wanapokutana na