Mstari wa Kukariri: “Msiwaogope wale wauao mwili, lakini hawawezi kuua roho; afadhali mwogopeni yule awezaye kuangamiza roho na mwili pia katika Jehanamu” Mathayo 10:28.
Masomo ya Biblia ya Kila Siku: Matendo 21:15-36; Matendo 21:37-22:21; Matendo 22:22-23:11; Matendo 23:12-35; Matendo 24; Hesabu 6
Usomaji wa Maandiko: Matendo 21:15-26
Utangulizi:
Paulo anakuwa mfungwa katika somo hili na anabaki kuwa mfungwa wa Warumi katika sehemu zote za Kitabu cha Matendo. Akiwa mfungwa wa Waroma, Paulo anapewa nafasi kadhaa za kujitetea mbele ya viongozi. Sisi pia tunaitwa