Andiko la Maandiko: Yakobo 5:13-18
Mstari wa Kukariri: “Ikiwa watu wangu, walioitwa kwa jina langu, watajinyenyekesha, na kuomba, na kunitafuta uso, na kuziacha njia zao mbaya; basi, nitasikia kutoka mbinguni, na kuwasamehe dhambi yao, na kuiponya nchi yao.” 2 Mambo ya Nyakati 7:14
Lengo la Somo: Kuelewa mamlaka na nguvu ya maombi.
Maombi ni muhimu kwa mwamini. Kwa sababu ya umuhimu wake katika maisha ya Kikristo, hatuwezi kusisitiza kupita kiasi hitaji na faida za maombi. Ni muhimu kwa Kanisa, huduma yake na ndugu wanaohudumu. Wanafunzi walitoa