Mstari wa Kukariri: “Basi jueni ya kuwa Bwana, Mungu wenu, ndiye Mungu; Mungu mwaminifu, ashikaye agano na rehema kwao wampendao na kushika amri zake, hata vizazi elfu;” —Kumbukumbu la Torati 7:9
Usomaji wa Maandiko: Zaburi 107:1-22
Utangulizi:
Uzoefu wa kugusa moyo zaidi unaoweza kutokea katika maisha ya kiroho ya mtu ni pale anapoingia katika agano na Muumba wake. Hili ni lazima tufanye tukiingia katika uhai wa milele na Mungu, kwani hakuna uhai ujao unaowezekana bila Mungu. Baba yetu wa Mbinguni si nguvu isiyo na utu; Yeye ni mtu ambaye katika mfano wake