Mstari wa Kukariri: “Njooni sasa, tusemezane, asema Bwana; dhambi zenu zijapokuwa nyekundu sana, zitakuwa nyeupe kama theluji; zijapokuwa nyekundu kama bendera nyekundu, zitakuwa kama sufu.” —Isaya 1:18
Usomaji wa Maandiko: 1 Petro 1:13-25
Utangulizi:
Agano jipya ambalo Mungu aliahidi kufanya na Israeli ni la kibinafsi, si la kitaifa, na kukubalika na kuitii ni mambo ya kibinafsi. Ingawa dhambi iliwatenganisha wanadamu na Mungu, Yeye hawalazimishi kumrudia. Mradi tu asili ya dhambi inawatawala wanadamu, hawawezi kuthamini uwepo wa Mungu. Adamu alipotenda dhambi aliogopa