Andiko la Maandiko: Yohana 14:5-26
Mstari wa Kukariri: Tumaini halikatishi tamaa, kwa sababu upendo wa Mungu umekwisha kumiminwa mioyoni mwetu na Roho Mtakatifu tuliyepewa sisi. Warumi 5:5
Lengo la Somo: Kutambua kusudi la ubatizo wa Roho Mtakatifu na athari yake kwa wapokeaji.
Tunasoma katika Waebrania 6:4-5 kwamba wale waliofanywa washirika wa Roho Mtakatifu wameonja nguvu za ulimwengu ujao. Tumeunganishwa na nguvu ambayo ni ya kizazi kijacho, lakini hiyo inapatikana kwetu sasa.